WAJUE WALIMU WA KISWAHILI WASHINGTON DMV!


Mwalimu Mkuu wa darasa la Kiswahili. Mwl. Mkumbuka akipata picha ya pamoja na Mwl. Iris Zielske mara baada ya kusaini mikataba ya kufundisha watoto wa Kitanzania kwenye darasa la Kiswahili, DMV pale College Park, Maryland mapema wiki iliyopita.
               
Walimu  wa darasa la Kiswahili wakipata picha ya pamoja katika maandalizi ya kufunguliwa kwa darasa la Kiswahili, darasa lianaoratibiwa na Jumuiya ya Watanzania hapa DMV. Kutoka kushoto ni Mwalimu Bernadeta Kaiza, Mwl. Iris  Zielske,   Mkuu, Lucia Mkumbukwa, na Mwl Asteria Hyera. Darasa yatafunguliwa siku ya Jumamosi Oct. 19, 2013, saa tisa (3:00pm) pale University of Maryland, College  Park. Walimu Asha Nyang'anyi na Mama Anna Mukami (hawapo pichani) hawakuhudhuria mkutano huo.

Wakiwa na nyuso za furaha ni walimu wa darasa la Kiswahili hapa DMV mara baada ya mkutano wao ulioweka mikakati ya namna ya kuliendesha darasa hilo kwa ufanisi. Kutoka kushoto ni Mwalimu Mkuu, Lucia Mkumbukwa, Mwl. Bernadeta Kaiza, Mwl. Asteria Hyera na Mwl. Iris  Zielske ambaye ni mwalimu mpya kabisa  aliyejiunga na madarsa ya Kiswahili mwezi huu.