MISS TABATA 2012- YAANI MWAKA HUU NI KIBOKO..MSHINDI WA MISS TANZANIA NATABIRI ATATOKEA TABATA:


WAREMBO...WAKIJINADI NADI MBELE ZA MASHABIKI PALE WEST PARK TABATA

WATCH OUT FOR THAT GIRL.......NATABIRI..THAT ONE...

WAREMBO WAKI TUMBWIZA...YAANI UREMBO KUMBE KAZI ANGALIA MATUMBO YAO WEE.

RATIBA KAMILI YA MAZISHI YA "STEVEN KANUMBA" KESHO HII HAPA...MAKAMU WA RAISI KUWA MGENI RASMI


                             
Mpangilio wa ratiba na nafasi itatolewa kwa kila mtu mwenye kuhitaji kushiriki mazishi ya Kanumba, kufanya hivyo katika tukio la kihistoria la kumsindikiza ndugu yetu huyo kwenye maisha ya milele. Hivyo, wito unatolewa kwa kila mtu kujitokeza kwenye shughuli nzima.

RATIBA
Mwili wa marehemu Steven Kanumba utachukuliwa kwa msafara kutoka Hospitali ya Taifa, Muhimbili saa 2:30 asubuhi. Utapitishwa Barabara ya Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi hadi Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni ambako Misa ya kumuombea itasomwa pamoja na salamu mbalimbali kabla ya watu wote kumuaga.

Wito unatolewa kwa watu kujitokeza kwa wingi kuanzia 
Saa 2:00 asubuhi, wakijipanga kando ya Barabara za Umoja wa Mataifa na Ali Hassan Mwinyi ili wautolee heshima mwili wa Kanumba wakati ukitolewa Muhimbili kwenda Leaders Club.

Saa 3:30 asubuhi, mwili wa Kanumba utapokelewa Viwanja vya Leaders, ukitanguliwa na mapokezi ya wazazi wake, viongozi mbalimbali wa serikali ambao juu yao kabisa atakuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohamed Gharib Bilal.

Saa 4:00 asubuhi, itakuwa ni muda wa kusoma Misa ambayo itachukua dakika 60, saa 5:00 kitakuwa kipindi cha salamu kutoka kwa watu mbalimbali.

Saa 6:00 mchana, ratiba ya kumuaga Kanumba itaanza mpaka saa 9:00 alasiri na baada ya hapo, utakuwa wakati wa kuusafirisha mwili kwa msafara kutoka Leaders Club mpaka Makaburi ya Kinondoni, msafara ukipita Barabara ya Tunisia, utakatisha Barabara ya Kinondoni kuelekea makaburini.

Saa 10:00 alasiri, mazishi yatafanyika kwa kufuata utaratibu wa imani ya marehemu.

Kamati ya Mazishi inatoa wito kwa watu watakaohudhuria shughuli ya kumzika ndugu yetu Kanumba, kuja na maua ili kumuaga kwa heshima.

Utulivu, unyenyekevu na ustahimilivu ni mambo muhimu yanayohitajika katika kipindi chote cha kumuaga mpendwa wetu Kanumba.

Bwana alitoa, Bwana ametwaa. Sisi wote tulimpenda kwa dhati na tulitamani aendelee kuwa nasi siku zote ila Mungu aliyemleta kwa mapenzi yake ameamua kumchukua. Jina lake lihimidiwe.

50 CENT" TO ACT ALONG SIDE "ARNOLD SCHWARZENEGGER IN THE NEW MOVIE "THE TOMB"


     
Rap mogul 50 Cent is getting more looks on his acting resume. He has just been added to the cast of the Sylvester Stallone filmThe Tomb. The story centers around the world’s most protected prison. Stallone’s character created the prison and must outsmart himself when he is sent there for a crime he didn’t commit.
Details regarding 50 Cent’s involvement are scarce. However, we do know he will join an already star studded cast. In addition to Stallone, 50 Cent will act opposite Arnold Schwarzenegger, James Caviezel, Vincent D’Onofrio, Amy Ryan, and Vinnie Jones. hopefully, he doesn’t wind up playing a prisoner or something stereotypical.

SUPER MODEL-NAOMI CAMPBELL..NOT CLOSE TO MARRYING THE BILLIONAIRE.


                       
Last month side chicks everywhere got their hopes up when their patron saint Naomi Campbell appeared to be one step closer to sealing the deal with her billionaire boyfriend after his wife finally got fed up and filed for divorce .
False alarm side chicks. The divorce is not going down…Ekaterina and Vladimir Doronin will not be divorcing any time soon.Despite reports that Ekaterina — the long-estranged wife of the Russian billionaire and property mogul — was finally ready to file for divorce and would name her hubby’s model girlfriend Naomi Campbell as a cause of their split, sources close to Ekaterina say that couldn’t be further from the truth.
“She has no plans to file for divorce in the near future,” a friend of Ekaterina told Page Six. “She hasn’t met with a lawyer as of yet. Vladimir takes very good care of her and her daughter [Katia, 15], and they both have very separate lives.”Vladimir and Ekaterina were married nearly 25 years ago, but they had already been living apart for a decade when Vladimir first met supermodel Campbell at the Cannes Film Festival in 2008.
“Ekaterina and Vladimir have been separated at least 10 years, and though he is with Naomi, they are all good friends,” our source said.Ekaterina was in New York this week looking for a pied-à-terre, although she plans on keeping her main home in London. She’s in the market for a palatial pad in the $20 million range. We’re told Doronin is paying for the Manhattan manse.

"KANUMBA" NA "DMK" ENZI ZA UHAI WAKE...I WILL ALWAYS MISS YOU!

 
                  DMK- KUSHOTO AKIPATA PICHA NA KANUMBA PAMOJA NA WADAU



                                                                DMK-KULIA -AKIWA PAMOJA NA KANUMBA

RATIBA YA MAZISHI YA KANUMBA KESHO JUMANNE!

                     
Habari zilizotufika hivi punde kuhusiana na mazishi ya aliye kuwa muigizaji nguli wa Filamu Tanzania marehemu Steven Kanumba 'The Great' ni kwamba Jumanne tarehe 10 April 2012 kuanzia saa 4 (nne) asubuhi mpaka saa 9 (tisa) mchana mwili wa marehemu Steven Kanumba utakuwa viwanja vya Leaders (Leaders Club) kwa ajili ya kuagwa na baada ya hapo mwili wa marehemu utaelekea katika makaburi ya Kinondoni ambapo ndo safari yake ya mwisho itakapo ishia. Mazishi yatafanyika saa 10 jioni (kumi) makaburi ya Kindondoni.  

PICHA YA "LULU" MSANII ANYEDAIWA KUSABABISHA KIFO CHA "STEVEN KANUMBA"


Habari za muda huu zinaeleza kuwa Jeshi la Polisi limeanza kumhoji 'mtoto' anayeshukiwa kuwa chanzo cha Steven Kanumba (The Great), Elizabeth Michael, maarufu kwa jina la kisanii, Lulu, amekanusha kumsukuma msanii huyo nguli hadi kufa.Amesema kamwe hakufanya hivyo, pamoja na kwamba walikuwa wamekwaruzana kwa muda mfupi na akaenda kuoga, akiwa anatoka bafuni alianguka (aliteleza) na kugonga kichwa kabla ya kukutwa na umauti.
Binti huyo ameiambia Polisi kwamba Kanumba (ambaye wamekuwa na uhusiano naye wa mapenzi kwa muda sasa) alikuwa 'amebugia' ujazo mkubwa wa pombe kali aina ya Jack Daniels (JD). Uchunguzi bado unaendela.