MAELFU WAJITOKEZA TAMASHA LA WA AFRICA WASHINGTON DMV - MAREKANI

Tamasha Hili la "FEST AFRICA" hufanyika kila mwaka katika Jiji la Silver Spring ambapo Mwaka huu Tanzania iliwakilishwa vyema kama inavyooneka na Bendera ya Tanzania ikiwa ya Kwanza kabisa mkono wa kulia.Tamasha hili lilifanyika Jumamosi na Jumapili katika Viwanja vya Veterans Plaza Silver Spring jumapili kama inavyoonekana kwenye picha ndio ilikuwa siku yenyewe haswa.Mbali na Chakula cha Kiafrica ambacho hupatikana kwenye tamasha hilo,pia Mitindo ya Mavazi ya kiafrica pamoja na utamaduni na muziki wa kiafrica na ngoma za asili huonyeshwa.



                Mwanamuziki  LORRAINE KLAASEN kutoka South Africa ndiye aliyekonga nyoyo za maelfu ya watu waliohudhuria.Mbali nakuimba nyimbo zake mwenyewe Mwanamuziki huyo aliimba nyimbo mbali mbali zilizowahi kutamba Afrika ya Kusini zilizoimbwa na wanamuziki kama Miriamu Makeba,Yvone Chaka Chaka,Brenda Fassie na wengine wengi.

        LORRAINE KLAASEN akiwajibika jukwaani huku watu wakirikaruka bila kupata nafasi ya kukaa chini kwa masaa yote mawili aliyokuwa Jukwaani.





IMG_3247
Emmerson Mwanamuziki kutoka Sierra Leone  akitumbuiza kwa madaha kabisa akijivunia Uafrica wake ndani ya Marekani.
IMG_3479
Kikundi cha Ngoma za Asili kikitumbuiza
IMG_3423
Mwanadada Naomi kutoka Cameroon alikonga nyoyo za watu.
IMG_3269
IMG_3300
Mitindo ya Mavazi ya Kiafrica iliwarusha roho maelfu ya watu waliojitokeza huku mamodel wa Kiafrica wakizidi kujichukulia Umaarufu katika Jiji la Washington nchini Marekani.
IMG_3321