DIAMOND SHOW HOUSTON TX MAY 25...RED CARPET YA NGUVU..PAPARAZZI WAKUMWAGA..TANGAZA BIASHARA YAKO KWA BEO POA!

TANGAZA  BIASHARA YAKO KWA BEI POA KWENYE RED CARPET AMBALO LINASADIKIWA KUWA LITAVUNJA RECORD ZOTE ZA WANAMUZIKI WA EAST AFRIKA WALIOWAHI KUJA AMERICA..
PIGA SIMU # 301-661-6207 : 240-605-1870 : 713-373-6525
TICKET ZA SHOW INGIA WWW.DIAMONDUSATOUR.COM

NAY AVUNJA NDOA YA SKAINA WA BONGO MOVIE



Nay wa Mitego 
Skaina
SASA hakuna ubishi kuwa, ile ndoa iliyofungwa kwa mbwembwe na kuvunjika kabla ya mwezi mmoja kati ya msanii wa filamu za Kibongo, Skyner Ally ‘Skaina’ na Saad Omar, chanzo ni Mwanabongo Fleva, Emmanuel Eribaliki ‘Nay wa Mitego’. 
Habari za awali zilisema kuwa, ndoa ya Skaina iliingia mdudu baada ya mumewe kugundua kuwa alinunua ‘mbuzi kwenye gunia’, kwani bidada huyo alikuwa na ujauzito wa mtu mwingine.
Hata hivyo, minong’ono ilikuwa inasema kuwa, mimba hiyo ilikuwa ya Nay ingawa awali, hakuna aliyekuwa tayari kufafanua kuhusiana na ishu hiyo.