RATIBA YA MAZISHI YA KANUMBA KESHO JUMANNE!

                     
Habari zilizotufika hivi punde kuhusiana na mazishi ya aliye kuwa muigizaji nguli wa Filamu Tanzania marehemu Steven Kanumba 'The Great' ni kwamba Jumanne tarehe 10 April 2012 kuanzia saa 4 (nne) asubuhi mpaka saa 9 (tisa) mchana mwili wa marehemu Steven Kanumba utakuwa viwanja vya Leaders (Leaders Club) kwa ajili ya kuagwa na baada ya hapo mwili wa marehemu utaelekea katika makaburi ya Kinondoni ambapo ndo safari yake ya mwisho itakapo ishia. Mazishi yatafanyika saa 10 jioni (kumi) makaburi ya Kindondoni.