PENNY AMFANYIA SURPRISE BIRTHDAY DINNER MAMA DIAMOND aka MAMA NASEEB AKE.



Penny akimlisha cake mama mkwe wake aka Mama Naseed 
 na baada ya tukio hili Diamond Platnumz amefunguka na kuandika yafuatayo kupitia blog yake:
"Hadi sasa nashindwa kuelewa lakini ntaelewa tu......ni mapenzi ya
dhati juu ya mama yangu mzazi.....
Siku ya jana ilikuwa siku njema kwangu na kwenye maisha yangu,ni
siku ambayo mama yangu mzazi
amezaliwa 7.7....
Kutokana na majukumu na kazi kuingiliana nilishindwa kufanya
chochote kama mnavyojua nilikuwa
na kibarua kizito kinanisubiri uwanja wa taifa kwenye tamasha la
matumaini so nsingweza kufanya
vitu viwili kwa wakati mmoja.....
Lakini chakushangaza kabisa nimewasili usiku na crew
yangu natokea kwenye show
nikakuta nimeachiwa kipande cha keki sikuelewa imetoka
wapi kwa kuwa mihadi yangu na mama yangu
ilikuwa ni Jumatatu ya leo kumpeleka kula chakula cha jioni
kusherekea siku yake hiyo kutokana na
majukumu ya kazi kuingiliana....
Nilichostajabishwa ni hiki na kufurahishwa sana mpaka
 kufikia machozi kunilenga
ni pale nilipokutana na picha hizi na kuziangalia.....
Kiukweli nilikuwa sijui chochote na hadi hapa navyoandika naona kama ndoto....
Nimejaribu kumuuliza mama yangu nae anasema akutambua
 kama kingekuwa kitu hiko laasha
alipigiwa simu kwenda kwa mazungumzo ya biashara kati
yake na Peniel na ghafla kukuta
familia na marafiki wakimsubiri wakiongozwa
na PENIEL MUNGIRWA aliyefanya usiku wa mama
 yangu kuwa wa furaha kabisa....
Shukrani za zati kwake kwa moyo wa ukarimu na mwenyezi
 mungu azidi kumzidshia na amfanyie
wepesi wa kila jambo lake la kheri......
Nami nikaona nisishuudie pekee yangu basi na wewe shabiki
yangu tuangalie wote kilichojiri pale Protea hotel,masaki jijini
Dar es salaam.....!!"