BEN POL- ASEMA WALE WATOTO KWENYE VIDEO YAKE MPYA SIO WATOTO WA MTAANI.....!!


 Kitaani kumeibuka tetesi kwamba wale watoto walioonekana kwenye video mpya ya Ben Pol inayoitwa MANENO kuwa wale ni watoto wa mtaani. Sasa kutokana na maswali kuwa mengi nikabidi nimtafute Ben Pol na kumuuliza juu ya hili na yeye akanijibu hivi...Namnukuu
"Wale watoto kwanza amewatafuta producer wake Karabani, mimi nilichokifanya nilimlipa gharama zote za kila kitu, na yeye ndo aliyekwenda kuongea na wazazi wa wale watoto mnaowaona halafu wale sio watoto wa mtaani wale wana nyumbani kwao wale na wawili pale ni ndugu  so walitengenezwa tu kidizaini,"

Nikamuuliza je vipi ulipata nafasi ya kuwaona au kukutana nao maana kwenye ile video kama umeonekana vipande vichache sana tofauti na video zingine anaonekana mwanzo mwisho
"Yeah niliwaona na nikapiga nao story na pia wao walikuwa wanatamani kuniona, na siku moja tulishoot wote, kama video ukiitizama pale darajani mimi nilikuwa juu ya daraja na wao walikuwa kwa chini. Kuonekana ndio nilionekana kidogo ili kuweka maana ya wimbo kwa kuonekana vitendo wafanyavyo watoto wa mtaani ambao ni yatima"


HABARI HII KUTOKA KWA DJ CHOKA !!