Family Day Bonanza la Skylight Band ndani ya kiota cha Escape One palikuwa hapatoshi Jumapili hii

IMG_0339
Nguvu kazi ya Skylight Band ikiongozwa na Sam Mapenzi kutoa burudani kwa mashabiki wa Band hiyo ndani ya kiota cha Escape One kwenye Family Day Bonanza kila siku ya Jumapili kuanzia Saa 10 jioni kwenye hewa safi na upepo mwanana wa Baharini.
IMG_0334
Superstar Mboni Masimba na rafiki yake nao walikuwepo kwenye kiota cha Escape One kupata burudani ya Skylight Band.
IMG_0326
Mdogo mdogo wadau walianza kujisogeza pande zile.
IMG_0323
Eneo kubwa la kujinafasi kwenye kiota cha Escape One ukiamua kukaa gorofani haya wewe tu na chaguo lako.

OMMY DIMPOZ APAA LEO KUELEKEA TANZANIA NDANI YA BUSINESS CLASS YA EMIRATE !


OMMY DIMPOZ AKIWA NDANI YA EMIRATE BUSINESS CLASS AKIELEKEA TANZANIA
Mwanamuziki wa Bongo Flava aliyemaliza Tour yake ya kwanza nchini marekani Ommy Dimpoz ameondoka leo kuelekea Tanzania ambapo ana show inamsubiri kesho usiku
Dimpoz akiwa Na USA Tour Manager wake "DMK" wakiwa Airport huku akiwa amepozi na Kofia yake ya POZ KWA POZ "PKP" Kofia hizo zinapatikana kwa special orders only.
Kushoto ni Promoter na Tour Manager "DMK" Pamoja na (kulia)Mwanamuziki Mtanzania aishie Marekani "AJ UBAO" Wakiwa Airport Walipo Msindikiza Ommy Dimpoz(katikati)
Ommy Dimpoz amewashukuru Tanzania Wote kwa kumsupport na pia Kuwaambia miji ile ambayo hakupata nafasi ya kuitembelea kuwa wakae mkao wa kula kwani atarudi kwa part two mwezi december, Tour Yake hiyo Part two itakuwa katika miji ya New York, Dallas, Oakland Chicago na Boston, Pia aliwashukuru Mapromota wake kwa kumkatia Business Class ili aweze kupumzika vizuri akiwa safarini kwani ana Show Dar es salaam mara tu baada ya kutua anaenda moja kwa moja kwenye Show..BONGO FLAVA IKO JUU!

KIJIWE CHA UGHAIBUNI BY VIJIMAMBO!

USHER AJITAYARISHA KIMAZOEZI KWA AJILI YA KUPIGANA NA SUGAR RAY !

article-0-18A3230D00000578-230_634x419
                 
                     article-0-18A3231100000578-67_634x835

                       article-0-18A3230900000578-913_634x858
Usher yeye ana mpango wa kupigana ndondi na bingwa (Legend) Sugra Ray Leonard katika filamu ijayo ya stone.Usher amekuwa akijifua kisawsawa ili kuhakikisha kuwa mwili wake unafanana na role atakayocheza kwani kupigana na Sugar Ray hata kama ni kwa kuact si mchezo.Ukifuata Diet inayotakiwa pamoja na mazoezi utaweza kuwa na mwili kama huu!

NEW VIDEO-BABY FACE AND TONI BRAXTON

babyface-toni-braxton

ILE VIDEO MPYA YA LUCCI "SUMU" SASA NDIYO HII !

THE GAME SASA KUWA LABEL MOJA NA DRAKE NA LIL WAYNE !

                       
                            THE GAME AKIWA NA OMMY DIMPOZ HOLLYWOOD
Kama tulivyo waletea wiki iliyopita Kutoka jijini Los Angeles wakati DMK Global na Swahili TV walipokutana na kuzungumza na The Game wakati wa Ziara ya Ommy Dimpoz kule California kuwa Rapper  huyo anategemea kujiunga na Cash money,Habari hiyo sasa imetimia baada ya CEO wa Cash Money records Birdman kutweet habari hiyo na The Game kumjibu let's go get them Niggaz.
    Kwa hiyo kwa sasa The Game officially ni lable mate wa Drake,Nicki Minaj,Lil Wayne,Bow Wow na wengine wengi.

BONGO MOVIE TUTAFIKA KWELI???


   Kweli Bongo Movie Tutafika kweli??
Mwanadada Irene Uwoya amepost Picha hii kwenye Instagram yake akionyesha kuwa alikuwa Location akishoot Movie.Tatizo ni kwamba katika picha hiyo inamuonyesha jambazi aliyemvamia Irene nyumbani kwake lakini kabla ya kuvamia alivua Viatu.
   Je tangulini jambazi akaogopa kuchafua nyumba aliyoivamia,Director wa Movie hii ni nani?????

LUCCI KUDONDOSHA "SUMU" YAKE TAREHE 13 OCTOBER!


Ikiwa ni takribani mwezi mmoja umepita toka producer wa audio wa studio ya Transformax, Luciano Gadie Tsere maarufu kama Lucci aachie video ya duet yake na mrembo Jokate Mwegelo ‘Kaka/Dada’, producer huyo anategemea kuachia video mpya ya wimbo unaoitwa ‘SUMU’. Director Nisher ambaye jina lake linaendelea kukua kutokana na kazi anazoendelea kufanya ndiye aliyehusika kuandaa Video hiyo ya SUMU.Kama Flyer hiyo inavyoonyesha Siku moja tu imebaki.Tembelea hapa kesho kujionea mwenyewe hiyo SUMU.

FROM NIGERIA "P-SQUARE SASA KUTUA BONGO NOVEMBER 23!

002.JP

004.JP
    Mtangazaji wa East Afrika Radio, Hillary Daudi (Zembwela)akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kutangaza ujio wa wasanii wa muziki wa kizazi kipya Peter na Paul Okoye maarufu kama  P – Square  kutoka nchini Nigeria pamoja na mdhamini Mkuu,Tarehe 23 Mwezi ujao ndipo watawasili nchini. Wasanii hao wataambatana na wasanii wengine 13 kutoka nchini humo. Pamoja nae katika Picha ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasilino wa Vodacom Tanzania Kelvin Twissa ambo ndio wadhamini wa onesho hilo.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Hyatt jijini Dar, Hillary Daudi wa East Afrika Radio, Amesema onesho hilo litakuwa la kipekee. P- Square wataongozana na wasanii wengine 13 ambao watatoa burudani ya Live Band siku hiyo Pamoja na wasanii wengine kutoka Tanzania.Wote tunatambua namna kundi hili linavyofanya vizuri ndani na nje ya bara la Afrika, licha ya kutoa burudani kwa mashabiki, pia litatoa fursa kwa wasanii wa ndani kujifunza kutoka kwa wasanii hawa vijana ambao wamepata mafanikio makubwa kutokana na kazi yao ya muziki,” alisema na kuongeza “hii itakuwa ni fursa ya kipekee kwa wasanii wetu wa bongo kujifunza kwa kuangalia wenzao wanavyofanya kazi”. Tutaendelea kuwaletea Habari zaidi za tour hiyo.